Leo kuanzia majira ya saa 3:10 asubuhi
kumezuka vurugu jijini Mwanza kati ya wafanyabiashara ndogondogo
al-maarufu kama Wamachinga na Jeshi la Polisi Mwanza kwa wafanyabiashara
hao kudai kufukuzwa eneo lao la biashara tofauti na makubaliano, hali
iliyosababisha watu kaadhaa kujeruhiwa na wengine watatu kuhofiwa
kupoteza maisha.Kamanda Sirro akielekea eneo la tukio kutoa amri ambayo kwa kiasi ilirejesha amani.
Magari
mawili ya mfanyabiashara maarufu mkoani hapa Mukeshi vunja bei
yamechomwa moto na kuteketea, vibanda kadhaa vimevunjwa, Baadhi ya
bidhaa zilizopangwa nje zimeibiwa nayo matairi yamechomwa katikati ya
njia panda kuingia mtaa wa Makoroboi kuelekea Soko kuu na kiunganishi
cha barabara ya Lumumba Mwanza huku baadhi ya wamachinga hao wakirusha
maboksi yaliyoshika moto kwenye majengo yaliyo karibu na eneo hilo kwa
nia ya kuyachoma moto.
Friji ikiteketea..
Vibaka
wamepora bidhaa na mali zilizokuwa nje ya Nono Super market nakisha
kuchoma friji ilokuwa na vinywaji ambavyo walivinywa kabla ya
kuiteketeza.
Kusanyiko la shaka-shaka.
Matairi
pia yamechomwa mbele ya lango kuu la soko kuu la jijini Mwanza
haliiliyopelekea kufungwa kwa soko hilo nazo biashara kusitishwa..
Wafanyabiashara wakichungulia yanayojiri nje kupitia lango kuu la soko kuu.
Kona
ya kuingia barabara ya Msikiti wa Ijumaa kutokea barabara ya Nyerere
risasi zimelia nao wananchi wakikimbia kujihami na mabomu ya machozi.
Market Street hakuna shughuli inayofanyika kwa sasa kwani hata vibaka wametumia mwanya huu kufanya uporaji.
Mtaa wa makoroboi kulikoanzia vurugu hakuna biashara inayofanyika maduka yote yamefungwa.
Machinga
na jiwe lake mkononi tayari kulirusha..Hali imekuwa tete kwa watanzania
wenye asili ya kiasia kwani imekuwa wakionekana tu wanafanyiwa kitu
mbaya.
Kuvunjwa vioo kwa jengo hili la msikiti wa hindu ni moja kati ya hasara zilizojitokeza.
Mpaka
sasa hivi ikiwa ni saa 6:15 barabara ya Nyerere haijatulia kwani kuna
umati mkubwa wa watu eneo hili mawe yakirushwa nayo mabomu ya machozi
yakisikika mitaa ya Makoroboi, Alhamini, Maketi na Msikiti wa Ijumaa
kuwatawanya waandamanaji.
No comments:
Post a Comment