Kipa
wa Barcelona Victor Valdes amesema amecheza na wachezaji wote wawili Ronaldinho
na Lionel Messi lakini kwa asilimia 100 anaamini Gaucho alikuwa mchezaji mwenye
kipaji kikubwa kuliko wote ambao amewahi kuwashuhudia akiwemo Messi. Kipa huyo
mwenye miaka 30, aliiambia Terra TV. Akiwa anatajwa sana kama mmoja ya
wachezaji bora kabisa kuwahi kutokea ulimwenguni, Messi ameuwasha moto kwenye
La Liga katika kipindi cha miaka 8, akivunja rekodi mbalimbali ikiwemo ya
kufunga mabao mengi. Lakini, Valdes anaamini Ronaldinho kipekee zaidi
aliibadilisha historia ya Barca alipowasili Nou Camp 2003, na kuchangia kwa
mafanikio wanayoyapata kikosi cha sasa. "Siku zote nimekuwa nikisema kwamba
Rony aliibadilisha historia ya klabu alipokuwa akicheza hapa. Alikuwa kiongozi
wa timu ambayo ilibadilisha histori yetu. "Hatukuwa tumeshinda taji lolote
kwa miaka mingi. Alikuja na kuifanya Barca kuwa na nguvu na kuifanya kuwa klabu
kubwa inayojulikana duniani kote kwa uwezo wake. Namshukuru sana kwa hilo.
Naweza kusema ndio mchezaji mwenye kipaji kikubwa kuliko wote ambaye nimewahi
kushea nae chumba cha kubadilishia nguo. Alikuwa anafanya vitu vyake vya
kustajaabisha kila siku.
No comments:
Post a Comment