Tuesday, July 10, 2012

JE CRISTIANO RONALDO ATAMSHINDA MESSI KWENYE TUZO YA UCHEZAJI BORA WA DUNIA 2012!!!!

Akiwa ameishi kwenye kivuli cha Lionel Messi kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita, labda mwaka 2012 ni nafasi nzuri zaidi kwa Cristiano Ronaldo kuvunja utawala wa 'mchawi wa Kiargentina' na kurudisha kwenye himaya yake tuzo ya mwanasoka bora wa dunia.

Mshambuliaji huyo wa Real Madrid alipoteza utawala wa tuzo ya mchezaji bora wa dunia tangu mwaka 2009 na kiukweli hajaonekana kama atakuja kuishinda tena tuzo tangu Messi aanze kufanya maajabu huku kikosi chake cha Barcelona kikitawala La Liga na mpaka nje ya mipaka ya Spain.

Lakini mwaka huu, kwa kuangalia mafanikio aliyoyapata Mreno huyu na kuwa na mafanikio finyu kwa Messi kutampa Ronaldo tumaini kwa mara nyingine tena kutajwa kuwa mchezaji bora na kunyakua Ballon d'Or.

Ronaldo alinunuliwa kwa ada ya uhamisho ya £80million iliyovunja rekodi kutoka Manchester United kwenda Real Madrid - huku akionekana tumaini jipya katikakurudisha siku nzuri kwa Los Blancos, lakini kwa bahati mbaya aliwasili Santiago Bernebau wakati ndege ya mafanikio ya kikosi cha Barcelona chini ya Pep Guardiola ndio ikianza kushika kasi kuruka.

Lakini hatimaye baada ya miaka mitatu na kufuatia kuongezeka kwa Mourinho kwenye timu ya Madrid, kila kitu kimeanza kurudi kwenye nafasi kwa Madrid na Ronaldo binafsi.

Ronaldo bila ubishi wala shaka ndio alikuwa star wa Real Madrid msimu uliopita huku wakishinda La Liga kwa pointi 100, tisa zaidi ya Barcelona na kuvunja rekodi waliyoiweka wenyewe kwa kuchukua ubingwa huku wakiwa na pointi 99.

Mreno anayevaa jezi namba 7 mgongoni alifunga mabao 46 kwenye ligi hiyo - zaidi ya nusu ya mabao aliyokuwa nayo mchezaji wa pili anayemfuatia kwa wachezaji wa Madrid  - Gonzalo Higuain aliyetia kambani magoli 22.

Mafanikio haya pia yakafunikwa na kivuli cha Messi, baada ya Muargentina huyo kutupia mabao 50 kwenye la liga.

Barani ulaya pia, Ronaldo  alicheza kwa kiwango kikubwa. Alifunga magoli 10 kwenye mechi 10 za Champions league huku Real wakitolewa kwenye nusu fainali kwa penati na Bayern Munich. Lakini kwa bahati mbaya tena pamoja na kucheza vizuri, Ronaldo alimaliza nyuma ya Mario Gomez aliyekuwa na magoli 12 - huku kwa mara nyingine tena Messi alikuwa juu yake kwa kumaliza kama mfungaji bora wa michuano hiyo kwa mara tatu mfululizo hiyo akiwa na mabao 14.

Hata baada ya msimu kuisha, Ronaldo bado alikuwa na nafasi nyingine ya kushindana ambayo Messi hakuweza kushindania: alikuwa na michuano ya kimataifa iliyokuwa njiani. Kuiongoza nchi yake ya Ureno kwenye michuano mikubwa ya Euro 2012.

Kufanya vizuri kwenye michuano hii kungemuhakikishia nafasi kubwa Ronaldo kushinda Ballon d'Or dhidi ya Messi.

Kwa bahati mbaya akaanza vibaya michuano hii kwa Ureno kufungwa na Ujerumani, kabla ya kucheza vibaya na kukosa nafasi nyingi za kufnga kwenye mchezo wa pili wa kundi la kifo dhidi ya Denmark, lakini wale wanaompinga Ronaldo aliwanyamazisha kwenye mchezo wa lazima kushinda na mwisho wa makundi dhidi ya timu ya Uholanzi. Mwanaume huyu alifunga mabao mawili ya ushindi huku akicheza kwa kiwango cha juu na kupelekea timu yake kuvuka kwa ushindi 2-1. Pia aliendeleza balaa kwenye mchezo wa robo fainali dhidi ya Czeh Republic kwa kufunga goli la ushindi na kuipeleka Ureno nusu fainali.

Ingawa, pamoja na kuweka rekodi ya kuwa mchezaji aliyepiga mashuti mengi kwenye lango la adui, na kumaliza akiwa amefunga mabao matatu sawa na mfungaji bora wa michuano hiyo Fernando Torres, Ronaldo atakumbukwa zaidi kwa michuano hii baada ya kushindwa kupiga penati ya mwisho kwenye mechi ya nusu fainali dhidi ya Spain.Ronaldo na kocha wake Paul Bento walicheza kamari ya kusubiri kupiga penati ya mwishodhidi ya Spain, lakini baada ya Moutinho na Bruno Alves kushindwa kufunga - Spain wakaimaliza mechi kabla ya Ronaldo hajapiga nafasi ya kupiga penati yake ya mwisho.

Mapema mwezi June, Messi - ambaye bado hajaonyesha kiwango chake cha klabu kwenye timu ya taifa - alicheza kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Brazil. Inaweza ikawa kweli ilikuwa mechi ya kirafiki, lakini kiwango alichoonyesha Messi kwa kufunga hat trick lilikuwa jambo la kukumbukwa. Goli la tatu la Messi litakumbukwa zaidi, alitoka nyuma na kuwapita mabeki kadhaa kisha kufunga kwa mkwaju mkali kulipelekea idadi ya jumla ya magoli yake kwa msimu 2011-2012 kufikia 82. Idadi ya kutisha sana.

Ronaldo anaweza akawa akashinda kikombe kikubwa kuliko Messi 2012, lakini atahitaji kucheza kwa kiwango chake kwa asilimia 100 na ku-deliver katika kipindi cha nusu mwaka kilichobaki ikiwa anataka kujihakikishia ushindi wa Ballon d'Or inayotolewa mwezi Desemba.

SUPER MARIO


LOVE & POWER : HII NDIO MOVIE YA MWISHO ALIYOICHEZA KANUMBA KABLA YA KUFARIKI.

                    
Nina uhakika bado hujaona Trailer ya movie ya mwisho ambayo Marehemu Muigizaji Steve Kanumba aliicheza, fahamu kwamba Trailer yake ndio hiyo hapo chini na movie inaanza kuuzwa muda wowote kuanzia sasa, hii ndio movie ambayo Director msaidizi aliefanya kazi na Kanumba kwa miaka saba alisema ilikua kama inatabiri kifo lakini siku chache baadae mwigizaji mkuu ambae ni Irene Paul alikanusha na kusema maneno ya director huyo hayakua na ukweli wowote, haifanani na jinsi kifo cha Kanumba kilivyotokea, movie inaitwa LOVE AND POWER.


'ONE & ONLY' Video - Navio

lifti ya mwamvuli

K-ZA & AGABIZOO (STATE CREW) - Mi Ni Soo.. prod by MTANI DA STUNNA

Bibi Cheka Feat. Godzilla - Good baba Felaa (Official Video)

Shilole feat. Kitokololo & Rich Mavoko - Viuno tucheze (Official Video)