Siku
mbili baada ya kuiwezesha klabu yake ya Chelsea kushinda kombe la mabingwa wa
ulaya kwa mara ya kwanza, mchezaji wa kimataifa wa Ivory Coast Didier Drogba
leo hii amewaambia wachezaji wenzie kwamba anaondoka Chelsea.
Shujaa
huyo wa Champions league amekiri kwamba hayupo tayari kukaa benchi.
Akiwa
na hisia kali Drogba, 34, alionekana kulia alipokuwa akiwaambia wachezaji
wenzie wa Chelsea uamuzi wake wakati wakiwa msafara wa kusherehekea ubingwa
mitaani jana.
Didier
ambaye mkataba wake unaisha mwezi ujao pale Stamford Bridge, ameliambia jarida
la France Football: "Hatutakuwa pamoja msimu ujao. Nilipoamua kuwaambia,
nilitaka niwaambie hivyo, lakini walinifanya nipotezee ujasiri. Hata hivyo ni
miaka mitatu sasa imepita tangu niseme nataka kuondoka - napata wakati mgumu
sana kukiri kwamba nimefikia mwisho kuwa hapa, lakini siwezi kukubaliana na
ukweli wa kukaa benchi na kuangalia wachezaji wengine wakicheza wakati klabu
itakapoamua kuja na mipango ya kutengeneza timu upya."
Drogba
ambaye amekuwa akihusishwa na kwenda kuungana na Anelka huko katika klabu ya
Shanghai Shenhua aliongeza: "Hivyo ndivyo ilivyo - najiandaa kwenda sehemu
nyingine ambayo sijaijua bado. Itakuwa kitu kingine tofauti."
No comments:
Post a Comment